Nilitazamia Robin kuondoka," alisema Sagna,"Lakini nilishangazwa na kuondoka Alex. Ana umri wa miaka 24, na alikuwa na miaka mitatu iliyosalia katika mkataba wake.Sagna alijiunga na Arsenal kutoka klabu ya Auxerre mwezi Julai mwaka 2007, na ameichezea Arsenal mechi 205.
Hivi sasa amepumzishwa, kwani bado anaendelea kupona baada ya kuvunjwa mguu katika mechi dhidi ya Norwich mwezi Mei.
Mkataba wake utakwisha mwisho wa msimu wa mwaka 2013-14, na alipoulizwa kama kuna yeyote ambaye ameshauriana naye kuhusiana na mkataba mpya, alisema "La, hakuna yeyote aliyezungumza nami."
No comments:
Post a Comment