imeandikwa na sauti ya amerika
Serikali ya Syria inalaumu  kile inachoita magaidi waliokuwa na silaha 
kwa mauaji ya kikatili ya zaidi ya raia 108 siku ya  Ijumaa karibu na 
mji wa Homs. Lakini mashahidi wengi wanasisitiza kuwa vikosi vinavyounga
  mkono serikali ndivyo  vilifanya mauaji hayo ya kikatili. Maandamano 
yenye jazba juu ya mauaji ya raia yaliyofanyika  Ijumaa huko Houla 
yanaendelea kote nchini Syria hiyo jana, ikiwa ni pamoja na mji mkuu 
Damascus  ambako vikosi vya uslama vilishambulia kwa risasi waandamanaji
 katika mtaa wa Midan. Msemaji wa wizara ya masuala ya nchi za nje wa 
Syria Jihad Makdissi aliwaambia waandishi habari kuwa jeshi la Syria 
halina lawama  juu ya  shambulizi la Ijumaa akisema wakulaumiwa ni 
magaidi waliokuw ana silaha. Mashambulizi hayo yalifanywa kwa saa  tisa 
ambapo pamoja na mauaji, nyumba zilichomwa moto na mali kupora.
 
No comments:
Post a Comment